Skip to main content

SABABU ZINAZOPELEKEA SHULE YA MSINGI KIZOTA KUTOKUWA NA UFAULU MZURI

Imeelezwa kuwa uhaba wa madarasa shuleni wanafunzi kutofika shule kwa wakati kutohudhuria darasani wakati wa vipindi na utoro, ni changamoto zinazosababisha ufaulu mdogo na hivyo kushuka kitaaluma kwa mwanafunzi.


Hayo yamebainishwa na mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Kizota iliyopo manispaa ya Dodoma Bi Olimpia Mpunga  wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya sababu za shule hiyo kushuka kitaaluma.

Mwl Olimpia amesema upungufu wa vyumba ya madarasa unawafanya wanafunzi  kusoma kwa awamu ili kupeana nafasi,  jambo ambalo ni changamoto kubwa.

Mwalimu Olimpia  amebainisha kuwa sababu zinazosababisha kuwepo kwa utoro kwa wanafunzi shuleni hapo ni pamoja na  wanafunzi  kuwa na makundi mitaani  na wengine kuwa na visingizio vya kuwa na matatizo .

Aidha amesema tayari wanao mpango mkakati wa kudhibiti utoro huo kwa kushirikiana na shirika la WWU ambao linashirikisha wazazi na walimu na kuwa kazi ya wazazi ni kujadili mbinu za kutumia katika kudhibiti utoro na mbinu za kuleta maendeleo katika taaluma.

Kwa upande wao wanafunzi wamewaasa wanafunzi wenzao ambao wamekuwa na tabia ya utoro kwenye vipindi na wengine kutohudhuria shuleni kuwa ni vyema wakajijengea mazoea ya kwenda  shule kwani wasipohudhuria vipindi darasani hukosa uelewa wa baadhi ya masomo na hivyo kufeli katika mitihani yao ya mwisho

Rweikiza katebalirwe                                                         Dodomafm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...