Skip to main content

RAIS MAGUFULI KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA RELI YA KISASA DODOMA.

                                    Image result for rais magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anatarajiwa kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa mradi wa reli ya kisasa na ya mwendo kasi, katika kipande cha kutoka Mororgoro kuelekea mjini Dodoma .

Akiongea na Dodoma FM  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge amesema kuwa zoezi hilo litafanyika mapema kesho machi 14 katika eneo la kituo cha reli cha Ihumwa nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Amewataka wananchi mjini hapa kujitokeza kwa wingi ili kumuunga mkono rais Magufuli kwani reli hiyo itawasaidia wakazi wa Dodoma  kupata ajira, sanjari na kuongeza wawekezaji watakaotokana na urahisishaji wa usafirishaji wa bidhaa utakaokuwa ukifanywa na Treni ya kisasa.

Aidha DK Mahenge amewatoa hofu wananchi juu ya namna ya kufika katika eneo la Ihumwa akisema kuwa kutakuwa na treni zitakazobeba wananchi kuwapeleka katika eneo husika huku akitaja ratiba na muda wa treni hizo kuondoka itakuwa ni majira ya usiku.

Hata hivyo kituo hiki kimezungumza na baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma ambapo wamesema kuwa mradi huo utasaidia kurahisisha suala la usafiri kutumia muda mfupi ukilinganisha na usafiri wa magari huku wengine wakimuomba Mh.Raisi kutumia fursa hii kutatua changamoto mbalimbali zilizopo mkoani Dodoma .

Na Alfred Bulahya                                                         Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...