Skip to main content

RAIS MAGUFULI AZINDUA MAGARI 181 KATIKA BOHARI YA DAWA MSD YATAKAYOSAFIRISHA DAWA MIJINI NA VIJIJINI

                                  Image result for RAIS MAGUFULI ATOA MAGARI 181



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli amewataka viongozi wa dini kutumia madhabahu yao kuhamasisha ujenzi wa viwanda ili kuepusha matumizi makubwa ya fedha za kununulia dawa nje ya Nchi.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo katika hafla fupi ya ugawaji wa magari 181 ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya kusambaza dawa maeneo mbalimbali Nchini hafla iliyofanyika leo katika eneo la keko Jijini Dar Es Salaam.

Rais magufuli amesema zoezi la ununuaji wa dawa nje ya nchi linasababisha Nchi kupoteza fedha zaidi ya Sh. Bilioni 500 kila mwaka, fedha ambazo zingebaki Nchini ili kuchangia katika masuala mengine iwapo viwanda vya kuzalisha dawa Nchini vingekuwepo.


Aidha Mh. Rais Magufuli amelipongeza shirika la Global Fund kwa jitihada zake katika kuendelea kutoa huduma ya vifaa tiba kwa wananchi wa Tanzania na kwamba misaada hiyo inachangia kwa kiasi kikubwa kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amesema kwa sasa chanjo za watoto zinapatikana kwa kiwango kikubwa Nchini huku mkurugenzi wa bohari ya dawa nchini (MSD) Laurian Bwanakunu akiweka wazi kuwa bajeti ya dawa kwa mwaka 2017/18 imechangia kusambaza dawa zenye thamani ya sh. Bilioni 18 kila mwezi.

Bohari kuu ya dawa (MSD) ina jumla ya kanda za maghala yapatayo kumi nchini kote ambazo zinatumika kuhifadhia dawa.
Na Pius Jayunga                                                          Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...