Skip to main content

RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASA DODOMA - MOROGORO

Image result for ujenzi wa reli ya kisasa dodoma to morogoro


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli leo ameweka jiwe la msingi ujenzi wa reli ya kisasa 'Standard Gauge' katika eneo la Ihumwa Mkoani Dodoma.

Katika hotuba yake Rais Magufuli amesema ujenzi wa reli hiyo unatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa mizigo na abiria kwa wakati tofauti na ilivyo katika reli ya zamani ambayo huchukua masaa zaidi ya 11 hadi 12 kwa kutumia reli iliyopo.

Aidha Rais Magufuli amesema moja ya changamoto zinazolikabili Bara la Afrika ni pamoja na kukosekana kwa miundombinu imara na ya uhakika kwa ajili ya usafirishaji na kusababisha gharama za usafiri kuwa juu tofauti na mabara mengine Duniani.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo Waziri mkuu Kasimu Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya tano itaendelea kusimamia miradi yote ya maendeleo kwa kuzingatia ilani ya chama cha mapinduzi na kuwasihi wananchi kuwa wasimamizi wa karibu katika miradi hiyo.

Awali akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi huo mkurugenzi mkuu wa shirika la reli Tanzania TRC Bw. Masanja Kadogosa amesema ujenzi wa reli hiyo ni sehemu ya pili yenye vipande vitano kutoka Dar es salaam hadi Morogoro kilometa 300, Morogoro, Dodoma hadi Makutupora kilometa 422, Makutupora hadi Tabora kilometa 244, Tabora hadi Isaka kilometa 134, na Isaka hadi Mwanza kilometa 441.

Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya pili ya reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Dodoma katika eneo la Makutupora ulisainiwa mwaka 2017 kwa gharama ya dola milion. 1.923 sawa na Trilioni 4.3 za kitanzania ikijumuisha kodi ya Serikali huku ujenzi huo ukitarajiwa kukamilika ndani ya miezi 36 kuanzia februari 26 mwaka huu.

Na Pius Jayunga                                                    Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...