Skip to main content

RAIS MAGUFULI AKABIDHIWA RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG),

                                   


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa TAMISEM kuwasimamisha kazi wakurugenzi  wa Halimashauri mbili  kwa kuongoza kuwa na hati chafu Nchini.

Rais Magufuli amefikia uamuzi huo leo Ikulu Jijini Dare S Salaam baada ya kupokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad ripoti iliyobaini mapungufu katika halmshauri hizo juu ya zoezi la ukusanyaji wa mapato.

Waliosimamishwa kazi ni pamoja na Bw. Boniface Nyambe aliekuwa mkurugenzi wa Halamashauri ya Kigoma Ujiji, Bw. Daud Mlahagwa aliekuwa Mkurugenzi wa Halmshauri ya Pangani ili kupisha uchunguzi juu ya taarifa hiyo.

Aidha Rais Magufuli ameikabidhi taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) kwa Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa na kuagiza kupitiwa kwa taarifa hiyo kipengele kimoja baada ya kingine kupitia Baraza la Mawaziri, Ma Naibu mawaziri pamoja na makatibu wakuu wote wa wizara.

Awali akikabidhi taarifa hiyo kwa Mh. Rais mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) Profesa Mussa Assad amesema kuwa deni la Taifa linafikia Sh. Trilioni 46 kutoka Sh. trilioni 41 la mwaka jana, na kwamba ni ongezeko la asilimia 12, huku akishauri kufanyika ufuatiliaji katika baadhi ya taasisi zilizopewa ripoti ya ukaguzi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa ameahidi kufanyia kazi ushauri uliotolewa na wenyeviti wa kamati za Bunge ili kuhakikisha madhaifu yaliyojitokeza taarifa hiyo hayajirudii tena katika kipindi kijacho.

Na Pius Jayunga                                                      Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...