Skip to main content

NYUMBA ZA UDONGO ZABOMOKA KUFUATIA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA MJINI DODOMA


                                 Image result for NYUMBA KUBOMOKA ENEO LA CHINYOYA DODOMA


Nyumba 62 na vyoo 41 zilizojengwa kwa tofali za udongo zimebomoka kuta zake kutokana na mvua inayoendelea kunyesha mkoani Dodoma katika mtaa wa chinyoya kata ya kilimani manispaa ya Dodoma huku watu zaidi ya 300 wakiwa wameathirika na mvua hizo.

Akizungumza na kituo hiki baada ya kuzungukia mtaa huo na kufanya tathmini ya maafa hayo diwani wa kata hiyo ya kilimani  Neema Mwaluko,amesema kutokana na maafa hayo tayari amewasiliana na uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Dodoma mjini na mbunge wa jimbo hilo na kutoa taarifa juu ya maafa hayo.

Mbunge wa jimbo la Dodoma mjini Anton Mavunde ametoa msaada wa unga kilo 300 na sukarai kilo 75 huku diwani huyo akiomba watu wengine kuweza kuwasaidia wananchi hao walioathirika na hali hiyo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo wa chinyoya Faustina Bendela amesema kubomoka kwa nyumba hizo kunatokana na mtaa wake kutokuwa na mifereji ya kutolea maji na barabara za kudumu na mtaa huo bado haujapimwa hivyo wananchi kutoshindwa kujenga nyumba bora na imara .

ukiangalia Dodoma sasa ni makao makuu ya serikali na huku mtaa wake ukiwa na zaidi ya wananchi 3500 kwa sensa ya mwaka 2012,ambapo mpaka sasa idadi  ya watu imeongezeka kwa wananchi wengi kuhamia katika mtaa huo.

Ikumbukwe kuwa miezi miwili iliyopita katika zoezi la usafi katika mtaa huo  mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk.Binilith Mahenge,alitoa agizo kwa mkurugenzi wa manispaa ya Dodoma kuhakikisha mtaa huo unafanyiwa mpango wa upimaji ili wananchi wa mtaa huo waweze kujenga ujenzi wa nyumba bora ili kuendana na hadhi ya makao makuu.

Na ANIPHA RAMADHAN                                          DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...