Skip to main content

NGOMA ANAENDELEA KUIMARIKA KAMBINI YANGA MOROGORO KUELEKEA MECHI NA SINGIDA JUMAPILI

MSHAMBULIAJI Mzimbabwe wa Yanga SC, Donald Ngoma anaendelea kuimarika katika kambi ya timu hiyo mjini Morogoro kujiandaa na mchezo wa Robo Fainali ya Azam Sports Federation (ASFC) Aprili 1, mwaka huu.

  Yanga watakuwa wageni wa Singida United katika Robo Fainali ya mwisho ya Azam Sports Federation Jumapili Uwanja wa Namfua mjini Singida na katika kujiandaa na mechi hiyo wameweka kambi Morogoro.

  Majeruhi wa muda mrefu, Ngoma ni miongoni mwa wachezaji waliopo kambini Morogoro na Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kwamba Mzimbabwe huyo anaendelea vizuri.

                       

Saleh amesema Ngoma ameshiriki mazoezi na wenzake kikamilifu kwa siku zote mbili chini ya kocha Mkuu, Mzambia George Lwandamina.

 
Meneja huyo amesema kwamba Ngoma amekuwa akifanya mazoezi yote yanayotolewa na kocha wake ikiwa kupiga mashuti,  mipira ya faulo pamoja na mbinu za kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo huo.

 
"Ngoma anaendelea vizuri, ameungana na wenzake kwa kufanya mazoezi ya pamoja, kufuatia majukumu ya benchi la ufundi," alisema.

 
Meneja huyo alisema hali ya kambi ipo vizuri pamoja na kufanya mazoezi mara mbili kwa siku ikiwemo asubuhi na jioni.

 
Donad Ngoma aliumia Septemba 30, mwaka jana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

 
Kuhusu hali ya mshambuliaji mwingine majeruhi wa muda mrefu, Mrundi, Amissi Tambwe, Saleh amesema kwamba mchezaji huyo anaendelea na mazoezi mepesi ya viungo mjinj Dar es Salaam ataungana na wenzake timu hiyo itakaporejea kutoka Singida.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...