Skip to main content

MWADINI ALLY AMWAGIWA SIFA BAADA YA MECHI YAO DHIDI YA SINGIDA UNITED

                              Image result for MWADINI ALLY PICHA 

BAADA ya kuonyesha uwezo mkubwa kwenye mchezo dhidi ya Singida United, Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor Cheche, ameweka wazi kuwa hali ya kutokata tamaa mazoezini na uzoefu ndivyo vilivyomng’arisha kipa Mwadini Ally kwenye mtanange huo.

  Mwadini aliyeingia kwenye kikosi cha kwanza cha Azam FC kwa mara ya kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu msimu huu dhidi ya Singida baada ya Razak Abalora kusimamishwa na Bodi ya Ligi, alifanikiwa kuonyesha kiwango bora kabisa akiokoa michomo mingi ya wachezaji wa Singida hasa kipindi cha pili.

  Cheche alisema kipa huyo ni moja ya makipa wazoefu na kufikichua amekuwa akifanya vema kwenye mazoezi ya kila siku ya timu hiyo.

 

“Mchezaji unamwangalia kwenye mazoezi wachezaji wetu wengi wa kiswahili (Kitanzania) wanapokuwa hawachezi mechi ya kwanza na ya pili na ya tatu anakuwa hafanyi jitihada kwenye mazoezi lakini Mwadini (Ally) toka tumeanza msimu katika mazoezi yuko vizuri n ahata mtu akija anaweza kujiuliza kwa nini hapati nafasi ya kucheza.

 
“Kwa sababu nafasi ya golikipa akishaanza mmoja anapofanya vizuri sio rahisi kumbadilisha lakini katika mazoezi amekuwa akifanya vizuri zaidi kila siku anapofanya kiasi kwamba ikitokea kitu ukimweka unakuwa huna wasiwasi,” alisema.

 
Aidha mbali na Mwadini kucheza mechi moja ya ligi, pia msimu huu amecheza mechi moja ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) dhidi ya Shupavu, ambayo Azam FC haikuruhusu nyavu zake kuguswa kwenye ushindi wa 5-0, mabao matatu ‘hat-trick’ yakifungwa na Paul Peter huku mengine yakitupiwa na Yahya Zayd na Idd Kipagwile.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...