Skip to main content

MTIBWA SUGAR KUWA KOSA WACHEZAJI WAWILI KUELEKEA KUCHEZA NA AZAM FC

TIMU ya Mtibwa Sugar ya Morogoro itawakosa wachezaji wake wawili, wote mabeki wa pembeni, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ na Salum Kanoni katika mchezo wa Robo Fainali ya Azam Sports Federationa Cup (ASFC) dhidi ya Azam FC kesho.

                           Image result for MTIBWA SUGAR IMAGE

Mtibwa Sugar watakuwa wageni wa Azam FC kuaniza Saa 2:00 usiku Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam katika Robo Fainali ya ASFC.

  Na kuelekea mchezo huo, Kocha wa timu hiyo Kocha Mkuu wa Mtibwa, Zuberi Katwila amesema kwamba wachezaji wake wengine wote wapo fiti ukiondoa mabeki wa zamani wa Simba, Baba Ubaya na Kanoni ambao watakosekana kesho.  


Akizungumzia mchezo huo, Katwila mchezaji wa zamani w Mtibwa, amesema; “Kila timu iliyofika hapa katika robo fainali ya kombe hili ni nzuri, hivyo tunajua tunaenda kupambana na timu  nzuri hivyo tunaenda tukijua tunapambana na timu nzuri ila tumejipanga kwa ajili ya kuwaletea furaha na heshima wana Mtibwa Sugar”.

 
Robo Fainali za Azam Sports Federation Cup zinaanza jioni ya leo, Stand United wakiikaribisha Njombe Mji FC Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

 
Kabla ya Azam FC kuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar kuanzia Saa 2:00 usiku kesho, Tanzania Prisons watakuwa wenyeji wa JKT Tanzania Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya na Aprili 1, Uwanja wa Namfua mjini Singida, Yanga watakuwa wageni wa Singida United

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...