Skip to main content

MKUU WA MKOA WA DODOMA AWAASA TARURA NA WAKANDARASI

                               Image result for mkuu wa mkoa wa dodoma



Mkuu wa mkoa wa Dodoma DR.BINILITH MAHENGE amewataka TARURA pamoja na wakandarasi kutumia fedha walizopewa ipasavyo katika matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2017/18 na  kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika katika miradi hiyo ili kutunza miundombinu.

Ameyasema hayo wakati wa Zoezi la utiaji saini mikataba ya miradi ya ujenzi wa  barabara kupitia TARURA  ambao ni wakala wa barabara za  mjini na vijijni  na wakandarasi  iliyofanyika jana katika ukumbi wa VETA kwa awamu ya pili kwa lengo la kuanza matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2017/18.

DR MAHENGE Amewahimiza wakandarasi waliopewa jukumu la kusimamia miradi hiyo kutengeza barabara kwa kiwango kilicho bora ili kuendelea kuimarisha miundombinu hapa nchini.

Mratibu meneja wa  TARURA mkoani Dodoma Bwana MOHAMAEND  MKWATA amesema kazi kubwa ya TARURA ni kuendelea kufanyia matengenezo mtandao wa barabaraza za mijini na vijijni na  Utekelezaji wa miradi hiyo ukizingatia mpango wa manunuzi na uwepo wa fedha kwa kuzingatia miradi husika.

Katika awamu ya kwanza TARURA mkoa wa Dodoma imeweza kufanikinikisha kusainiwa kwa mikataba ishirini na saba katika halimashauri za Bahi,Chamwino ,Kongwa na Dodoma Manispaa huku miradi 25 ikifanyiwa mchakato wa manunuzi
Katika awamu ya pili matengenezo yanatarajiwa kufanyika katika wilaya ya Mpwapwa,Chemba,Kondoa,pamoja na manispaa ya Dododma.

Na Mindi Joseph                                                       Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...