Skip to main content

MAYANGA ANAHUSISHWA KUFUKUZWA STARS AKIWA KAPOTEZA MECHI MBILI PEKEE, NI SAHIHI?

Kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga, anahusishwa kuondoshwa kuitumikia timu hiyo akiwa ameiongoza kucheza jumla ya michezo 16 tangu aanze kuifundisha.
Mayanga alitangazwa kukichukua kikosi cha Taifa Stars kutokea kwenye mikono ya Charles Boniface Mkwasa ambaye ni Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga kwa sasa.
                        

Ukiangalia rekodi za Mayanga, zinaonesha ameiongoza timu hiyo katika mechi 16 huku akiwa amepoteza michezo miwili pekee.
Mayanga vilevile ameenda sare michezo 7 tangu aanze kukinoa kikosi hicho cha Stars na akiwa ameshinda mechi 7.
Kwa rekodi hizi bado inaonesha Mayanga anapaswa kupewa nafasi ya kuendelea kukinoa kikosi cha Stars licha ya kushindwa kuipa mataji timu hiyo.
Wapo baadhi ya wadau wamekuwa wakieleza kutofurahishwa naye haswa katika uteuzi wa kikosi pamoja na timu inavyocheza kwenye mashindano wakidai kuwa kiwango hakiridhishi.
Yawezekana kutofanya vizuri pia katika mashindano mbalimbali ndiyo sababu ya Mayanga kulaumiwa na kuanza kuhusishwa aondoke.
Siku kadhaa zilizopita Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Wilfred Kidao, alinukuliwa akisema wameanza mchakato wa kumpata Kocha atakayechukua nafasi ya Mayanga.
Kwa kauli kama ile ukijumlisha na hizi za baadhi ya wadau wa soka zinaonesha kabisa kuwa Mayanga hapewi motisha ya kutosha kwenye nafasi yake kuendelea kuinoa Stars. Inadhihirisha ipo mashakani.
Nadhani ifikie wakati tujaribu kuwa na uvumilivu na si kutegemea kupata mafanikio makubwa ndani ya siku moja. Unaambiwa ng'ombe hawezi kunenepa siku ya mnada kama alikuwa hajapata marisho ya kutosha tokea utotoni.
Juzi hapa kaka yangu Haji Manara, alieleza kuwa inabidi taifa liitishe mjadala wa kujadili tatizo la timu yetu ya Taifa kushindwa kufanya vizuri ilihali ilishaleta 'Sampuli' ya kila Kocha kuinoa Stars.
Tatizo kubwa linaloikabili Stars kwa jicho la ndani ukija kutazama vizuri utagundua hata Makocha hawahusiki, vipi kuhusu ubora wa ligi yetu?
Tuna akademi za kutosha kuanzisha msingi wa soka kuanzia ngazi ya chini kabla ya kufika huku juu? Ni baadhi ya maswali ambayo tunapaswa kujiuliza.
Mipango inayofanywa kwenye Ligi Daraja la Kwanza, shutuma za baadhi ya viongozi kuzipandisha baadhi ya timu mpaka Ligi Kuu unadhani zitaweza kuleta matokeo chanya kwenye kikosi chetu?
Tuna wachezaji wachache sana ambao wanacheza soka la nje, na hatuwezi kuwategemea peke yao kuweza kuinua soka letu.
Ifikie wakati kuwe na mipango mikakati endelevu ya kuimarisha soka la vijana kuanzia mashuleni, haswa shule za msingi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo hamasa kubwa ilikuwa katika mashindano ya UMITASHUMTA iliyokuwa ikiibua vipaji vya wachezaji.
Tusimhukumu Mayanga wakati tulishakuwa na Makocha wengi walioifundisha Stars hata wasio wazawa. Tuangalie ligi zetu za ndani kwanza kama zinaendeshwa kiuhalali bila mipango mipango, figisu na rushwa ambayo inaua mpira wa nchi hii.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...