Skip to main content

MANISPAA YA DODOMA YAOMBWA KUHARAKISHA ZOEZI LA UPIMAJI WA MITAA ILI SHUGHULI ZA MAENDELEO ZIENDELEE

       Image result for mtaa wa chinyoya DODOMA

Imeelezwa kuwa kuchelewa kwa upimaji wa mitaa ndani ya manispaa ya Dodoma kunachangia kukwama kwa nguvu kazi kutoka kwa wananchi katika kujitolea kuboresha miundombinu mibovu katika baadhi ya mitaa .

Hayo yameelezwa na mwenyekiti wa mtaa wa chinyoya kata ya kilimani  manispaa ya Dodoma  Bi FAUSTINA BENDELA wakati akizungumza na Dodoma FM ambapo amesema kuwa  changamoto zinazoukabili mtaa wake zinasababishwa na kuchelewa kwa zoezi la upimaji wa mitaa.

Amesema zipo barabara mbovu na mifereji iliyoziba lakini uwawia vigumu wananchi kuweka nguvu kazi kwani bado mtaa huo haujapimwa na zoezi hilo linasimamiwa na halimashauri ya manispaa ya Dodoma licha ya awali mtaa huo kuwa chini ya mamlaka ya ustawishaji makao makuu CDA.

Aidha Bi FAUSTINA ameiomba halimashauri ya manispaa ya Dodoma kulichukulia uzito suala hilo la upimaji wa mitaa kwani uwepo wa miundombinu mibovu unasababisha kukwama kwa baadhi ya shughuli za maendeleo.

Katika hatua nyingine akizungumzia suala la ulinzi na usalama mwenyekiti huyo amesema kwa sasa hali ni shwari huku akimpongeza kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Dodoma  GILLES MUROTO kwa kuwa  amekuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa wenyeviti wa mitaa pale anapoombwa msaada.

Hata hivyo amewaomba wananchi wa mtaa wa chinyoya kuendelea kuitikia wito wa mikutano ya hadhara inayoitishwa kwa ajili ya kujadili maendeleo ya mtaa wao.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                  DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...