Skip to main content

MANISPAA YA DODOMA IMEKUJA NA MKAKATI WA KUPIMA TB KILA MGONJWA ANAYEINGIA HOSPITALINI


                                        Image result for MKOA WA DODOMA
Katika mapambano dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu manispaa ya Dodoma imeandaa mkakati mpya wa kuhakikisha kila mtu anayeingia hospital anapimwa ugonjwa huo.


Hayo yamebainishwa na mratibu wa ugonjwa wa kifua kikuu manispaa ya Dodoma Dokta Pelesi Lukango wakati akizungumza na dodoma FM kupitia kipindi cha taswira ya habari ambapo amesema tayari wameandaa fomu za usajili kwa kila eneo la hospitali kuhakikisha kila mgonjwa anayeingia anapimwa afya yake.

Hata hivyo dokta peles amesema kwa sasa changamoto ni kubwa ambapo kila mgonjwa anayeugua kifua kikuu hubainika na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI.

Amewataka wananchi kuhakikisha wanaenda kwenye vituo vya afya kupima na kutambua afya zao ambapo huduma hizo hutolewa bure bila malipo.

Hivi karibuni waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh,Ummy Mwalimu alinukuliwa akisema kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO takwimu zinaonesha kuwa watu 77 hufariki dunia kila siku nchini Tanzania kutokana na kifua kikuu  huku mkoa wa Dar –Es-Salaam ukitajwa kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 20.

Na Benard Filbert                                                   Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...