Skip to main content

MAMLAKA YA HALI YA HEWA SASA KUTENGEWA BAJETI YA KUTOSHA.


                                            Image result for MAMLAKA YA HALI YA HEWA


Serikali kupitia wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiliano imesema itaendelea kuwezesha mamlaka ya hali ya hewa nchini kwa kutenga bajeti ya kutosha ili kukabiliana na changamoto zilizopo katika mamlaka hiyo.

Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa baraza ya wafanyakazi wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania leo mjini Dodoma ambapo amesema serikali inatambua mchango wa mamlaka ya hali ya hewa hivyo itaendelea kuwezesha kuinua mtandao wa vituo vya mamlaka hiyo.

Prof.Mbarawa amesema mamlaka ya hali ya hewa imekua ikitoa mchango katika taifa na kwamba mamlaka hiyo imejenga kuaminika  kwa wananchi kutokana na taarifa zake zinatolewa na kuwataka kuongeza juhudi katika ufanyaji kazi wao ili waaendelee kuaminika.

Awali akisoma hotuba mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania Dr Agnes Kijazi amesema licha ya kuwepo kwa mafanikio katika mamlaka hiyo ikiwa ni pamoja na Tanzania kuwa nchi ya tatu barani Afika kupata cheti cha ubora bado wana uhitaji wa kubadilisha vifaa vinavyotumia zebaki ifikapo mwaka 2020.

Mariam Matundu                                                                  Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...