Skip to main content

MAKOCHA WAFUNGIWA BAAADA YA VURUGU

                     Related image 

Kamati tendaji ya chama cha soka mkoani dodoma imewafungiwa miezi sita  na kuwatoza faini  makocha wa vilabu vya gwassa nato ya chang’ombe na Watumishi ya mpwapwa kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo tukio la vurugu katika mchezo wa Gwassa dhidi ya watumishi


Kupitia taarifa  ya DOREFA kwa vyombo vya habari imesema kuwa  katika mchezo wa gwassa dhidi ya watumishi uliofanyika tarehe 18 mwezi wa 3 mwaka 2018 wameabaini matukio mbalimbali,1mashabiki kufanya vurugu,walimu wa timu mbili hizo kugombana,kumtukana msimamizi wa kituo,kocha msaidizi wa timu ya watumishi kuzuia wachezaji kutoendelea na mchezo,timu ya watumishi kugoma kuendelea na mchezo  na baadhi ya wachezaji kujihusisha na vurugu.


Kupitia kamati tendaji  ambayo imekata hapo juzi wamatoka na maamuzi ya timu ya gwassa pamoja na timu wa watumishi vimetozwa faini ya shilingi laki moja kila mmoja kutoka na msahbiki wake kuhusika na  vurugu na fedha hizo zinatakiwa kulipwa kabla ya michezo inayofutia.

Baada ya taarifa hiyo nilimtafuta mtendaji mkuu wa chama cha soka mkoani dodoma Hamisi kisoi Amesema kuwa kutoka na maamuzi hayo ,wataendelea kuhakikisha wanasimamia ligi hiyo kwa misingi ya usawa na uwazi na haki mpaka bingwa hapatikane

Pia tumezungumza na kocha wa Gwsaa nato Juma ikaba ambaye amefungiwa miezi Sita na kutozwa faini ya shilling laki moja amesema kuwa kutoka na maamuzi hayo ameyapokea hana budi kukubali juu ya hilo

Wadau wa soka wanasemaje juu ya maamuzi haya,super fortu ambaye pia ni katibu wa timu ya DFC yeye ni mdau wa soka ametoa pongezi kwa chama cha soka mkoani dodoma juu ya maamuzi hayo

NA SELEMANI JUMA

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...