Skip to main content

MAAFISA USTAWI NGAZI YA KATA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU YA WAJIBU WA MWANAUME KATIKA FAMILIA

             
                                         Image result for USTAWI WA JAMII


Maafisa ustawi wa jamii ngazi ya mkoa na halmashari wametakiwa kushirikiana na maafisa ustawi wa jamii ngazi ya kata ili kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya utekelezaji wa sera mbalimbali zinatomtaka mwanaume kutimiza wajibu wake katika familia.

Msemaji wa wizara ya afya maendeleo ya jamii, jinsia ,wazee na watoto idara kuu ya maendeleo ya jamii Erasto Ching’oro amesema ipo haja kwa maafisa ustawi wa jamii kuendelea kutoa elimu kwa jamii hususani wanaume kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Amesema kwa mujibu wa sheria ya ndoa sura ya 69 katika kifungu cha 63A kimempatia wajibu mwanaume wa kutunza familia yake kikamilifu na iwapo atapata matatizo ya kiafya busara na maridhiano katika familia yatafanyika ili kuendelea kuimarisha familia.

Amesema mbali na sheria hiyo ya ndoa ,sera ya maendeleo ya jinsia ya mwaka 2000 imesisitiza wajibu wa mwanaume katika kushirikiana na mwanamke ili kutunza familia kikamilifu.

Hata hivyo wazazi wote wametakiwa kutambua jukumu la kutunza familia kwa kutoa malezi bora kwa wototo wote pasipo kubagua jinsia ni jambo linalowezesha kuwa na familia bora.

Mariam Matundu                                                        Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...