Skip to main content

KITUO CHA MABASI YAENDAYO MIKOANI MJINI DODOMA KUANZIA KESHO KITAKUWA RASMI KATIKA KITUO KIPYA CHA NANE NANE NZUGUNI



                             Image result for stendi ya mabasi dodoma kuhamishwa   
Zoezi la uhamishaji wa Kituo cha Mabasi mkoani Dodoma linatarajiwa kukamilika kwa siku ya leo huku madereva ,abiria na wafanyabiashara wakilalamikia miundombinu ya kituo kipya.


Wakizungumza na Dodoma FM mapema leo baadhi ya wafanyabiashara  wamesema stendi ya Nanenane haiwafai kutokana na miundombinu kutoridhisha hali ambayo imepelekea kupangiwa muda wa kufunga kufanya biashara zao.

Nao Madereva wa mabasi wameeleza kuwa stendi ya Nanenane bado ni changamoto kwao  kwa sababu baadhi ya gari zitakuwa zinabeba abiria wote katika  stendi ya Sabasaba  na kupelekea wao kukosa abiria.

Hata hivyo baadhi ya abiria wamesema kutokan na kuhamishwa kwa stendi ya mkoa watakabiliwa na changamoto  ya  kuongezeka kwa gharama ya usafiri kutoka mjini hadi stendi ya Nanenane.

Dodoma FM imezungumza na Afisa habari wa manispaa ya Dodoma Bwana RAMADHANI JUMA ambae amekiri kuwa leo ni siku ya mwisho  kuhamishwa stendi hiyo na kwamba kuanzia  kesho shughuli zote za usafiri zitapatikana katika eneo la Nanenane Nzuguni.

Katika hatua nyingine amewataka wafanyabiashara,abiria na madreva kuwa wavumilivu kwani ni kipindi cha mpito  na tayari  manispaa inatarajia kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa eneo la NZUGUNI  pamoja na soko kubwa ambapo itachukua miaka miwili kukamilika.

Na,Mindi Joseph                                                            DODOMA FM 

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...