Skip to main content

JAMII YAHUSISHA UGONJWA WA UKOMA NA IMANI ZA KISHIRIKINA

                                            Image result for UGONJWA WA UKOMA


Wanajamii wameshauriwa kuacha kuhusisha ugonjwa wa ukoma na imani za kishirikina hali inayoweza kupelekea kuenea kwa ugonjwa huo kwa kiasi kikubwa.

Rai hiyo imetolewa na doctor Martin Masimba ambaye ni mratibu wa magonjwa ya kifua kikuu na ukoma mkoani Dodoma wakati akizungumza na Dodoma  fm kupitia kipindi cha Taswira ya habari.

Dokta Masimba amesema kuwa wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakihusisha baadhi ya magonjwa  na imani za kishirikina huku wakiufanya ugonjwa huo kukua zaidi.

Akizungumzia hali ya ugonjwa wa ukoma mkoani Dodoma dokta Masimba amesema kuwa maambukizi ya ugonjwa huo yamepungua tofauti na kipindi kilichopita,kutokana na jitihada zinazoendelea kufanywa na wizara husika.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wakizungumza na kituo hiki wamesema baadhi ya watu huhusisha imani za kishirikina na ugonjwa huo baada ya kushindwa kupona wanapotumia dawa za hospitali.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani Takwimu zinaonesha kwamba, katika kipindi cha mwaka 2015 kumekuwepo na maambukizi mapya ya Ukoma 212, 000 sehemu mbali mbali za dunia, lakini asilimia 60% ya waathirika wote walikuwa wanatoka nchini India  Brazil na Indonesia takwimu zingine ni kwamba, watoto walioambukizwa Ukoma ni asilimia 8.9% ya wagonjwa wote duniani na kwamba, asilimia 6.7 ya watoto wagonjwa walionesha mabaka mwilini wao!

Na Benard Filbert                                                    Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...