Skip to main content

DUWASA INATUMIA MILIONI 485 KWA MWEZIKUWAPATIA WAKAZI WA MANISPAA YA DODOMA HUDUMA YA MAJI

                                       Image result for AFISA MAWASILIANO DUWASA SEBASTIAN WARIOBA 
Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) inatumia Jumla ya shilingi milioni 485 kwa mwezi katika kuhakikisha huduma ya maji safi inawafikia kwa urahisi wakazi wa manispaa ya Dodoma.


Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kutoka mamlaka hiyo Bwana Sebastian Warioba ameyasema hayo wakati akizungumza na Dodoma FM  juu ya mfumo mpya wa ulipaji wa bili ya maji kwa njia ya simu.

Amesema kiasi hicho cha fedha kimegawanyika katika maeneo tofauti ikiwemo ulipaji wa nishati ya umeme unaotumika katika kuzalisha  na kusukuma maji hayo ili kuwafikia wananchi, malipo ya wafanyakazi pamoja na marekebisho ya mitambo ya usafirishaji wa huduma ya maji.

Aidha Bwana Warioba amesema (DUWASA) ndie mwenye jukumu la kufanya marekebisho ya miundombinu ya maji pale inapoharibika lengo ikiwa ni kuendelea kutoa huduma stahiki kwa wananchi na jukumu la mwananchi ni kutoa taarifa za uwepo wa uharibifu wa miundombinu hiyo ili kufanyika marekebisho na kuokoa upotevu wa maji.

Katika hatua nyingine Bw. Warioba amesema ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi mamlaka hiyo imeanzisha mfumo wa ulipaji wa kodi kupitia simu za kiganjani mfumo ambao unarahisisha kumpatia mteja taarifa mbalimbali za matumizi ya huduma ya maji.

Na Pius Jayunga                                                             Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...