Skip to main content

CAG ATOA UFAFANUZI JUU YA DENI LA TAIFA LINALOKADIRIWA KUFIKIA TRILIONI 46

               
                                       Image result for MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU HESABU ZA SERIKALI

Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Prof Mussa Juma Assad ametoa ufafanuzi juu ya uwepo wa makosa katika  ripoti ya ukaguzi ya mwaka wa fedha iliyowasilishwa kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT John Pombe Magufuli.

Akiongea na waandishi wa habari hii leo prof Assad amesema kuwa mnamo March 27, mwaka huu aliwasilisha ripoti zake za ukaguzi wa mwaka wa fedha ulioishia mnamo june 30/ 2017 kwa rais Magufuli ambapo ripoti hizo zilikuwa na dosari juu ya mwenendo wa deni la Taifa.

Amebainisha kuwa hadi kufikia June 30, 2017 deni la Taifa lilikuwa shilingi tirioni 46.08 ambapo kati ya deni hilo ,deni la ndani ni shilingi tirion 13.34 sawa na asilimia 29 na deni la nje ni shilingi tirioni 32.75 sawa na asilimia 71 hivyo deni la nje ni aslimia 31 ya pato la Taifa na kwamba kwa sasa deni la Taifa ni himilivu.

Akiendelea kutoa ufafanuzi kufuatia kauli yake wakati wa uwasilishaji wa ripoti hizo prof Assad ameomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa wananchi huku akidai kuwa matokeo ya ukaguzi wa ripoti hizo yatawekwa wazi kwa umma baada ya kuwasilishwa bungeni, tukio linalotarajia kufanyika kabla ya april 12 mwaka huu, katika kikao cha kwanza cha bunge kitakachofanyika baada ya ripoti za CAG kuwasilishwa kwa Mh Raisi.

Na Alfred Bulahya                                                      DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...