Skip to main content

BILIONI 896.3 ZIMETUMIKA KULIPA MADENI YA WATUMISHI WA UMMA

                              Image result for msemaji mkuu wa serikali






Jumla ya shilingi bilioni 896.3 zimetumika kulipa madeni ya watumishi wa umma wakiwemo wakandarasi pamoja na watoa huduma waliokuwa wakiidai serikali baada ya kukamilika kwa zoezi la kuhakiki madeni ya watumishi wa umma katika awamu ya kwanza.

Msemaji mkuu wa Serikali Dr. Hassan Abbas ameyasea hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofsini kwake Mjini Dodoma na kueleza kuwa adhima ya kulipa madeni hayo inatokana na ahadi iliyotolewa na Rasi Dr. John Pombe Magufuli kulipa madeni yote ya watumishi wa umma.

Amesema fedha hizo ni kati ya shilingi Trilioni 1 iliyotengwa na Serikali kwa ajili ya kushughulikia malipo ya watumishi wa umma wanaoidai serikali na baada ya kuhakiki madeni hayo katika awamu ya kwanza, zoezi hilo linaendelea tena katika awamu inayofuata.

Dr. Abbas amesema Serikali inaendelea na uhakiki wa madai ya watumishi wa umma ili kuhakikisha kuwa kila mtumishi anapatiwa stahiki yake na kila uhakiki utakapokuwa ukikamilika taarifa itakuwa ikitolewa kwa vyombo vya habari na watumishi hao wakipatiwa stahiki zao.

Katika hatua nyingine Dr. Hassan Abbas amesema Serikali inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa ambapo mabehewa 1590 pamoja na vichwa vya treni 25 vimekwisha kuagizwa sambamba na ujio wa ndege nne mpya hadi kufikia mwezi july mwaka huu ili kurahisisha usafirishaji wa anga.

Na Pius Jayunga                                                    Dodoma Fm Radio

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...