Skip to main content

BARAZA LA BIASHARA BAHI LAOMBA KUJENGEWA UWEZO ILI KUFIKIA UCHUMI WA VIWANDA


                Image result for WILAYA YA BAHI DODOMA


Baraza la biashara wilaya ya bahi wameomba kupewa elimu zaidi juu ya mradi wa uboreshaji wa mazingira ya biashara (LIC) ili kuwasaidia kuboresha biashaa zao.

Wajumbe hao wamesema elimu hiyo ikitolewa na kuwafikia wananchi itasaidia kuweza kuboresha biashara zao pamoja na  kupendekeza kuundwa kwa  kikosi kazi kitakachosaidia kuandaa mafunzo na kuandika maandiko ili kupata fedha za ufadhili.

Aidha wamesema licha ya wao kuwa na elimu lakini wapo wananchi ambao elimu hiyo haijawafikia hivyo wao wakianza kupewa elimu itasaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi wengine kwa urahisi na kuweza kuendana na Tanzania ya viwanda

Kwa upande wake Afisa biashara Wilaya ya Bahi Said Isike  ametaja changamoto zinazowakabili  katika uibuaji wa biashara kwa mwananchi mmoja mmoja kuwa  ni uandikaji wa maandiko ya kuwawezesha  kupata ufadhili, jambo ambalo ameahidi kulisimamia.

Kwa upande wake Mratibu wa mabaraza ya biashara Mkoa (TNBC) Joseph Nyaromba amewataka wajumbe hao kuona umuhimu wa chombo hicho ambacho kinatambulika kisheria  ili wakuze biashara zao na hatimaye wamsaidie Mh.Rais John Magufuli kuweza kufikia uchumi wa Viwanda.

Afisa mwandamizi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi kutoka mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma Barnabas Masika amesema kama mamlaka wapo tayari kushirikiana na wilaya hiyo katika kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kutosha juu ya ufanyaji biashara zao.

Mariam Matundu                                           Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...