Skip to main content

ASASI ZA KIRAIA ZAJENGEWA UWEZO WA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KWA JAMII

                                       Image result for NGONEDO


Imeelezwa kuwa  wanajamii wamekuwa hawatambui haki pamoja na wajibu wao juu ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo pamoja na kuwa na uwazi na uwajibikaji katika kutoa huduma hususani za kiserikali.

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za kiraia mkoani Dodoma (NGONEDO)  Bi, Sara Mwaga wakati akifungua mafunzo ya kujengea uwezo asasi za kiraia Wilayani Chamwino  yenye lengo la kujenga uwazi na uwajibikaji kwa jamii na katika kufuatilia na kuangalia maswala ya serikali za mitaa na taarifa mbalimbali za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali na utawala bora.

Bi Sara amezitaka asasi za kiraia kutumia mafunzo hayo vizuri kwa kuongeza ufahamu na kupata mbinu zitakazowawezesha kufanya kazi na kuwajibika katika kuliletea Taifa maendeleo.

Kwau pande wake Mratibu wa Asasi za kiraia Bw, Edrward Mbogo amesema kupitia asasi za kiraia zitakazoshiriki mafunzo hayo ya siku mbili asasi hizo zitasaidia jamii kwa kupeleka elimu waliyojifunza kwa vitendo huku akiishukuru serikali ya halmashauri ya Chamwino kwa kuunga mkono mafunzo hayo.

Akizungumza katika mafunzo hayo muwezeshaji kutoka chuo Kikuu cha Dodoma Dkt, Ajali Mustapha amesema asasi za kiraia zinafanya kazi kwa niaba ya jamii inayowazunguka na kwamba zinamchango mkubwa katika harakati za kiutawala, uwazi na uwajibikaji .

Kwa upande wao  washiriki wa mafunzo hayo  wamesema kumekuwa na changamoto nyingi katika jamii ikiwemo kutokutatuliwa changamoto zao kwa wakati kutokana na ufinyu wa bajeti .

Na Phina Nimrod                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...