Skip to main content

WAATHIRIKA WA VIRUSI VYA UKIMWI WAPATIWA FURSA ZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI



                                             








Waathirika wa ugonjwa wa virusi vya ukimwi  wameshauriwa kujiunga na taasisi  mbalimbali za uzalishaji mali ili kuondokana na unyanyapaa na suala la utegemezi.

Ushauri huo umetolewa na mratibu wa kupambana na ugonjwa wa ukimwi Manispaa ya Dodoma dokta Elias Nyoni wakati akizungumza na kituo hiki  ambapo amesema ni vizuri waathirika wa virusi vya ukimwi wakajiunga na taasisi mbalimbali ambazo zinajihusisha na uzalishaji kiuchumi.

Dokta Eliasi amesema kuna taasisi ambazo zinajihusisha na utoaji mikopo kwa waathirika wa virusi vya ukimwi lengo likiwa ni kuwasaidia kupata kipato kutokana na baadhi yao kukata tamaa na kujiona kama wananyanyapaliwa katika jamii.

Ameongeza kuwa matatatizo ya kunyanyapaa watu wenye virusi vya ukimwi bado yapo na hali hiyo hupelekea kuwakatisha tama waathirika hao huku akisema kuna baadhi ya waathirika wanajiweza kiuchumi na kufanikiwa kufanya mambo makubwa ya kimaendeleo katika jamii ikiwepo kuwapeleka watoto shuleni.

Akiongea na kituo hiki mmoja wa wakazi mkoani Dodoma Bwana Fidelis Leonard amesema ni vibaya kwa mtu yeyote kumnyanyapaa mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi kwani kwa kufanya hivyo hujihisi ni mtu asie na haki sawa na wengine.

Msemaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Glory Mziray hivi karibuni alisema Watanzania walioonesha kuwa na ufahamu sahihi wa elimu kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi wanafikia asilimia 60 jambo linalosababisha kuwepo mwamko mdogo wa kubadili tabia.
Na Benard Filbert                                             Chanzo :Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...