Skip to main content

UNAPOZUNGUMZIA SEKTA YA MAJI HUWEZI KUACHA KUGUSIA SUALA LA USAFI WA MAZINGIRA

 

SERIKALI imewataka wadau wa Sekta ya maji na usafi wa mazingira nchini kuisaidia Serikali katika kutekeleza vipaumbele vyake ambavyo ni ujenzi wa miundombinu ya maji,utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji na usafi wa mazingira.
 Hayo yameelezwa leo mjini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Dk.Tixon Nzunda,wakati akifungua mkutano mkuu  wa wadau wa uwajibikaji katika sekta ya maji na usafi wa mazingira(WASH).


 Naibu Katibu Mkuu huyo amesema ni muhimu wakati wote wadau kuisaidia Serikali katika kutekeleza malengo  badala ya wadau hao kuja na vipaumbele vyao visivyoendana na malengo ya Serikali.
 

Hata hivyo naibu katibu mkuu huyo hakusita kuzungumzia baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta ya maji nchini ikiwa ni pamoja na migongano ya maslahi huku akiwataka wadau hao kuziibua changamoto hizo.
 


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtandao wa maji na usafi wa mazingira(TAWASANET),Herbet Kashililah,amesema mkutano huo utawasaidia kujua changamoto ambazo zipo katika sekta ya maji na usafi wa mazingira.


 Mkutano huo  umeandaliwa na Mtandao wa maji na usafi wa mazingira(TAWASANET) ambapo wadau hao wanajadiliana changamoto zilizopo katika sekta ya maji na usafi wa mazingira pamoja na kubadilishana uzoefu katika sekta hizo.
Na Phina Nimrod     
                            

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...