Skip to main content

CHAMA CHA WALEMAVU(TOSODEFFA) CHAIOMBA SERIKALI KUREJESHA VYUO VYA WALEMAVU.


Chama cha walemavu TOSODEFFA mkoani Dodoma kimeiomba serikali kuanzisha tena kwa mara nyingine vyuo vya walemavu ambavyo vilikuwa  vimesitisha  mafunzo yake ili kupunguza ongezeko la walemavu  wanaoishi kwa kutegemea msaada.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa chama hicho Bwana Paul Manyika  alipokuwa akizungumza na taswira ya habari  ofisini kwake ambapo amesema kipindi cha awali kulikuwa na vyuo vingi vya walemavu nchini hivyo ilikuwa rahisi kwa walemavu kupata ujuzi mbalimbali na kujitegemea baada ya mafunzo lakini sasa hivi  vyuo vimepungua kwa kiasi kikubwa.

Akizungumzia kuhusu ukosefu wa ajira kwa walemavu nchini amesema ni changamoto inayowakabili na kupelekea ongezeko la walemavu ambao wanaishi mtaani bila kazi wakati baadhi yao wana uwezo wa kufanya kazi kwenye taasisi mbalimbali.

Pamoja na hayo amesema ni vigumu kwa mtu mwenye ulemavu kupewa msaada mara kwa mara ili aweze kukidhi mahitaji yake hivyo kungekuwepo na vyuo hivyo vingesaidia kumuandaaa mlemavu kutokutegemea kuajiriwa na hatimaye kutegemea kujiajiri katika sekta mbalimbali ikiwepo ufundi selemala,pamoja na ujenzi.

Wakizungumza na kituo hiki kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi akiwepo bwana Kitavian Gaspar amesema ni vizuri serikali ikajenga vyuo hivyo ili kusaidia watu wenye ulemavyu kujikwamua kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...