Skip to main content

MWENYEKITI ACT AMEKANUSHA UVUMI WA KUAMIA CCM





Mwenyekiti wa chama cha Act-Wazalendo Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma Bw. Masudi Bigangika amekanusha uvumi wa taarifa zilizokuwa zinamhusisha kukihama chama hicho na kujiunga na chama cha Mapinduzi (CCM).
Bw. Bigangika ameyasema hayo wakati akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu kufuatia uvumi ulioanza kuenezwa na baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi Wilayani humo kuwa mwenyekiti huyo amekihama chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi.
Amesema kuwa taarifa zilizotolewa na baadhi ya viongozi wa CCM Wilayani humo ni uvumi unaosambazwa kwa lengo la kumchafua yeye na chama chake licha ya kuwa yeye hayupo tayari kukihama chama chake cha ACT Wazalendo.

Aidha Bw. Bigangika amesema kutokana na wimbi la viongozi mbalimbali kuhamia chama cha mapinduzi huwenda ikawa ni moja ya sababu za kuzushwa kwa uvumi wa yeye kukihama chama chake na kukiri kuwa kutokana na kuenezwa kwa taarifa hizo kunaweza kuchangia kwa sehemu kubwa kudhoofisha wafuasi wa chama cha ACT wazalendo

Katika hatua nyingine Bw. Bigangika ametoa Wito kwa wananchi na wafuasi wa chama cha Act wazalendo kupuuza taarifa zinazotolewa na watu katika mitandao ya kijamii na badala yake watu wajenge mazoea ya kusikiliza kauli ya kiongozi husika ili kuepuka mkanganyiko miongoni mwa jamii.

Na Pius Jayunga                                               

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...