Skip to main content

MAAFISA ELIMU WATAKIWA KUFICHUA WALIMU WANAOKIUKA MAADILI

                        Image result for walimu kutongoza

Serikali imewataka maafisa elimu kote nchini kutowaficha waalimu wanaofanya vitendo viovu dhidi ya wanafunzi bali kuwabainisha ili wachukuliwe  hatua kwa mujibu wa sheria.
Hayo yameelezwa hii leo mjini Dodoma na waziri wa nchi,ofisi ya rais,tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo wakati akifungua kikao cha kazi cha  siku mbili cha maafisa elimu wa mikoa na wilaya  chenye lengo la kujadili mipango,malengo na mikakati ya uboreshaji elimu nchini.
 
Waziri Jafo amewaeleza kuwa  haridhishwi na  baadhi ya walimu ambao wamekuwa wakijihusisha  kimapenzi na wanafunzi kwani jambo hilo si tu linakiuka maadili bali pia ni chanzo cha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI.

Kupitia kikao hicho imemlazimu waziri Jafo kumuagiza naibu katibu mkuu wa TAMISEMI kuchunguza na kufanya maboresho ili  mkoa wa Dodoma  ambao ndio makao makuu ya nchi uweze kufanya vizuri

Kwa upande wake katibu mkuu wa wizara hiyo mhandisi Mussa Iyombe amewataka maafisa elimu kujitathimini iwapo wanaiweza kazi hiyo na kuacha tabia ya kuwatesa waalimu bali kutatua changamoto zao.

Kufuatia maagizo hayo mwenyekiti wa maafisa elimu wa mikoa na wilaya Mayasa Hashimu amesema kuwa watatekeleza maelekezo yote na kuahidi kutoka na maazimio ya kiutendaji katika kikao hicho.
 
Mariam Matundu     

      

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...