Skip to main content

KONGWA: UZAZI WA MPANGO UNATUSAIDIA KUJIKINGA NA WATOTO WALIOFUATANA

                                                Image result for uzazi wa mpango



Kina mama Wilayani Kongwa wametakiwa kufika katika vituo vya afya ili kupata maelekezo sahii juu ya matumizi ya njia bora za uzazi wa mpango kutokana na baadhi yao kutokuwa na uelewa. 

Akiongea na Dodoma FM Afisa Muuguzi na Mratibu wa Uzazi wa Mpango wa Wilaya ya Kongwa Bi. Lessy Mdegellah amesema wapo baadhi ya kinamama ambao wamekuwa wakisikia maneno ya upotoshaji kutoka kwa watu wasiokuwa na ufahamu juu ya njia za uzazi wa mpango hivyo amewataka kuondoa uoga na kufika katika kituo cha afya kwa ajili ya kupata maelekezo ya kitaalam.

Bi. Lessy amesema yapo maudhi madogo madogo kwa baadhi ya kina mama wanaotumia njia za uzazi wa mpango ambayo huisha baaada ya muda mfupi na kuwataka kina mama watakaokutana na maudhi hayo kufika katika kituo cha afya kwa ajili ya uchunguzi zaidi kutoka kwa wataalamu wa afya.

Sambamba na hayo Bi. Lessy amesema zipo faida mbalimbali za kutumia njia za uzazi wa mpango ikiwemo kumpa mama na baba nafasi ya kufanya shunghuli nyingine pamoja na kumpa mtoto nafasi ya kukua vizuri.

Wakizungumzia faida za kutumia njia za uzazi wa mpango baadhi ya kina mama wamesema kuwa zinawapa nafasi ya kuzaa kwa mpangilio pamoja na kuondokana na changamoto ya kuwa na watoto wengi waliofuatana kwa umri.

Wito umetolewa kwa baadhi ya kina baba wanaowakataza wake zao kutumia njia za uzazi wa mpango kuwaruhusu ili kuwapa nafasi ya kupumzika.

Na Phina Nimrod                                                                                      Chanzo:Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...