Skip to main content

JAMII IMETAKIWA KUTAMBUA UTOAJI WA ELIMU JUU YA KUEPUKA MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA



Jamii imetakiwa kutambua utoaji wa elimu kwa watanzania juu ya kuepuka matumizi ya madawa ya kulevya ni wajibu wa kila mtu ili kuondoa tatizo hilo nchini.

Akizungumza na kituo hiki sajent Cristian Mlelwa kutoka jeshi la polisi kitengo cha madawa ya kulevya mkoa wa Dodoma amesema kila mtu anawajibu wa kuelimisha jamii kuhusu kuepukana na matumizi ya dawa za kulevya ili kuongeza elimu katika jamii.
Sajent Cristian amesema wao kama jeshi la polisi wanawajibika kwa nafasi yao kuhakikisha kila mtanzania anapata elimu kuhusu madhara ya utumiaji wa dawa za kulevya.

Hata hivyo amesema katika sehemu ambazo wanaenda kutoa elimu ikiwepo mashuleni wamekuwa wanawatumia waathirika wa madawa ya kulevya kama mfano kuonesha kuwa wameacha madawa ya kulevya.

Kwa upande wake mwenyekiti wa vituo vya soba house nchini na aliyewahi kuwa muathirika wa madawa ya kulevya Bi Nuru amesema vituo  vya soba house vilivyopo nchini vinamsaada mkubwa kwa waathirika

Bi Nuru ameongeza kuwa tarehe 24 mwezi wa pili wameandaa mchezo wa mpira wa miguu utakaofanyika uwanja wa jamhuri mkoani hapa ambapo kutakuwa na uchangiaji wa damu.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...