Skip to main content

IDADI YA WATU WENYE MATATIZO YA AKILI NCHINI INAKADIRIWA KUFIKA ASILIMIA 1



Serikali imesema idadi ya watu walio na matatizo ya akili Nchini inakadiliwa kufika asilimia 1 na hii ni kutokana na wengi wao kuto kuhuduria katika vituo vya afya kwa ajili ya matibabu hatua inayochangia kukosekana kwa takwimu sahihi za idadi ya wagonjwa hao.

Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Faustine Ndungulile ameyabainisha hayo leo Bungeni mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali Mbunge Joseph Mbona Mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini alietaka kufahamu ni kwanini Serikali haina utaatibu wa kuwachukua wagonjwa wa akili mitaani na kuwapeleka katika hosptali za wagonjwa wa akili kupatiwa matibabu.

Amesema watu walio na matatizo ya akili kwa sehemu kubwa asilimia 48 wamekuwa wakienda kupatiwa huduma katika vituo vya afya, asilimia 24 wamekuwa wakienda kwa waganga wa kienyeji na walio baki hupelekwa katika tiba za kiroho makanisani na mikisikitini huku wengine wakionekana mtaani bila kuwa na msaada wowote.

Amesema sheria ya afya ya akili ya mwaka 2008 inawataka ndug, na jamii kuwaibua watu walio na magonjwa ya akili na kuwapeleka katika vituo vya kutolea matibabu kwa usimamizi zaidi ili kupatiwa matibabu huku sheria hiyo ikiweka bayana kuwa afisa wa polisi, afisa usalama, afisa ustawi wa jamii Wilaya pamoja na viongozi wa dini wanawajibu wa kumbainisha mtu yeyote anaelanda landa na kutishia amani na usalama ili kumfikisha katika vituo vya afya

Katika kikao hicho Mbunge Halima Bulembo amesema si kila mgonjwa wa akili analanda mitaani na kushauri Serikali kufanya utafiti yakinifu ili kupata takwimu sahihi za wagonjwa wa akili Nchini kwa kuzingatia takwimu za shirika la afya Duniani WHO.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...