Skip to main content

HITILAFU YA UMEME YASABABISHA HOSPITALI YA AGA KHAN KUTEKETEZA MALI NYINGI

       
                       
Image result for HOSPITALI YA AGA KHAN YAUNGUA







Moto mkubwa uliwaka hapo jana katika jengo la Hospital ya Aga Khani (Apolo Medical Centre) Mkoani Dodoma na kuteketeza baadhi ya mali huku chanzo cha moto huo kikielezwa kuwa ni hitilafu ya umeme.
Akizungumza wakati wa zoezi la uokoaji na uzimaji wa moto huo Kamishina Msaidizi wa Jeshi la zima moto na uokoaji Regina Kaombwe amesema walipokea taarifa za moto huo majira ya saa kumi na moja kasorobo jioni ambapo kwa haraka waliwahi eneo la tukio na kukuta jengo lote likiwa linawaka moto hivyo kuanza kuudhibiti .
Baadhi ya wahusika kutoka katika hospital hiyo wakiwemo wafanyakazi wamelishukuru Jeshi la Zimamoto na uokoaji kwa kuwahi eneo la tukio kadri ya uwezo wao licha ya vitu vingi kuteketea kwa moto.
Mashuhuda ambao ni wakazi na wafanyabiashara wa maeneo hayo wamesema walianza kuona moshi mkubwa katika hospital hiyo ndipo moto ukawaka.
 Hata hivyo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Dodoma lilifanikiwa kuuzima moto huo na hadi sasa haijajulikana thamani ya vitu vilivyoteketea huku jeshi hilo likitoa wito kwa wananchi pindi waonapo matukio ya moto kutoanza kuuzima taratibu bali wawasiliane na jeshi hilo kwa kupiga simu namba 114 kwa ajili ya uokozi.
Mariam matundu                                                 Chanzo Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...