Skip to main content

Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa raisi muungano na mazingira mh, January Makamba amezindua Kamati ya taifa ya ushauri wa mazingira mkoani Dodoma






Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa raisi muungano na mazingira mh, January Makamba amezindua Kamati ya taifa ya ushauri wa mazingira mkoani Dodoma lengo ikiwa kuishauri serikali kuhifadhi na kuendeleza mazingira nchini.

Akizungumza na wanahabari waziri January Makamba amesema kamati hiyo ina wajumbe mbalimbali kutoka serikalini akiwepo mkurugenzi wa misitu,mipango miji na wengine ili kuweza kuwapa ushauri wa kitaalamu waziri mwenye dhamana.


Amesema kwa kipindi kirefu ambapo kamati hiyo haijakutana kuna uharibifu mkubwa wa mazingira katika sehemu mbalimbali nchini huku viongozi mbalimbali wa kisiasa wakitoa matamko na maamuzi mbalimbali kuhusu mazingira pasipo utaalamu.


Hata hivyo amezitaka taasisi na wizara mbalimbali nchini kuitumia kamati hiyo juu ya masuala yanayohusu mazingira ambapo kamati hiyo inawajibu wa kuita wizara yoyote na kupokea taarifa juu ya uhifadhi wa mazingira katika sekta husika.





Wadau wa elimu wameombwa kushirikiana kwa pamoja kuinua elimu kwa mtoto wa kike ikiwa ni pamoja na kuwa  na miundombinu bora ya vyoo ambayo itamuwezesha  mtoto wa kike kujistiri vizuri hasa katika kipindi cha hedhi.

Akizungumza na kituo hiki mwalimu mlezi wa wanafunzi wa kike  kutoka shule ya sekondari kintiku Wilayani manyoni Maisala Mawala  amesema kuwa tatizo la kukosa miundombinu bora ya vyoo kunapelekea wanafunzi kushindwa kuhudhuria masomo kikamilifu hasa wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.


Kwaupande wake makamu mkuu wa shule hiyo Othumani Bakari amesema kuwa ili kuinua elimu kwa mtoto wa kike jamii inapaswa kuwajibika kuondoa vikwanzo vinavyomfanya mwanafunzi wa kike kushindwa kufanya vizuri katika masomo.


Baadhi ya wanafunzi wakike kutoka katika shule hiyo wamesema hali ya kukosa miundombinu bora ya vyoo katika shule yao inawafanya wasiwe huru pindi wanapokuwa katika siku za hedhi hali inayopelekea kushindwa kusikiliza kwa makini na kuelewa  wawapo darasani.

 

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...