Skip to main content

MHADHIRI CHUO KIKUU DODOMA, AOMBA SERIKALI IFANYE MAREKEBISHO VIGEZO VYA KUOMBEA MIKOPO (TCU)



Serikali imeshauriwa kufanya marekebisho kwenye vigezo vipya ambavyo vimewekwa na bodi ya mkopo nchini  kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili kumuwezesha kila mwanafunzi ambaye anasifa za kuendelea na chuo kikuu.
 Image result for BOOK
Ushauri huo umetolewa na mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dodoma bwana Paul Luisulie wakati akiongea na kituo hiki ambapo amesema kuna haja kubwa ya serikali kufanya marekebisho kwenye vigezo hivyo ambavyo vimewekwa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu ili kuepusha kutengeneza matabaka baina ya watanzania.


Aidha ameziomba serikali za wanafunzi wa elimu ya juu kufuatilia suala hilo ili kuleta haki sawa kwa kila mwanafunzi ambaye anasifa za kujiunga na chuo kikuu  anastahili kupewa mkopo na sio kuwatenganisha katika madaraja tofauti.

Hivi karibuni bodi ya mikopo ya elimu ya juu nchini imetangaza vigezo vipya kwa wanafunzi ambao wanatarajiwa kujiunga na vyuo vikuu kwa mwaka wa masomo 2017/2018.

Kwa upande wao wazazi mkoania hapa akiwepo bwana Paul Dickluck pamoja na Juma Msamilo wamesema ni vyema serikali ingefanya marekebisho vigezo ambavyo vimewekwa na bodi ya mikopo nchini ili kila mwanafunzi mwenye sifa ya kujiunga na chuo kikuu apatiwe mkopo ili aweze kunufaika na elimu hiyo.

Na Benard filbert                

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...