TATIZO LA UKOSEFU WA ELIMU YA BIASHARA KWA VIJANA
Ukosefu wa elimu ya biashara imetajwa kama sababu ya vijana wengi kuto kujishulisha na biashara yenye faida na manufaa.
Akizungumza na kituo hiki mmoja wa vijana ambao wamejiajiri Francis Christopher amesema sababu mojawapo inayowarudisha nyuma vijana nikukosa Elimu yauzalishaji wa bidhaa pamoja na uendeshaji wa biashara jambo ambalo limekuwa likiwarudisha nyuma kimaendeleo.
Pamoja na hayo amesema vijana wanatakiwa kujitambua nakujua nini cha kufanya kwa wakati jambo ambalo linaweza kupunguza tatizo la ajira hususani kwa vijana.
clip kijana.
KUELEKEA SIKUKUU YA IDD BEI ZA BIDHAA SOKO KUU MAJENGO BADO ZAPANDA NA KUSHUKA.
Na Dodoma Fm
Wafanyabiashara wa Soko Kuu Majengo Mkoani Dodoma wamezungumzia hali ya biashara katika kuelekea msimu wa sikukuu ya idd mnamo mwezi September ikiwemo bidhaa kushuka na zingine kupanda hasa ukilinganisha na msimu wa bidhaa husika na kupelekea wateja kuwa wachache.
Wafanyabiashara wa Soko Kuu Majengo Mkoani Dodoma wamezungumzia hali ya biashara katika kuelekea msimu wa sikukuu ya idd mnamo mwezi September ikiwemo bidhaa kushuka na zingine kupanda hasa ukilinganisha na msimu wa bidhaa husika na kupelekea wateja kuwa wachache.
Wakizungumza na kituo
hiki wafanyabiashara hao wamesema kuwa kulingana na maandalizi ya sikukuu hiyo
bei za bidhaa zimetofautiana kutokana na msimu wa bidhaa husika ikiwemo viungo
vya chakula kupanda na bidhaa nyingine kubaki bei yake ikiwemo nyama na mchele,
na bidhaa zingine kushuka bei ikiwemo viazi na mahindi.
Bw. Khalid Ally amebainisha
sababu mbalimbali za biashara sokoni hapo kuwa ngumu hasa kwa kipindi hiki cha
kuelekea sikukuu ya idd kuwa ni pamoja na kukosekana kwa wanafunzi wa vyuo.
Bei za bidhaa katika
msimu wa kuelekea sikukuu ya idd kwa sasa zimetegemea na msimu wa mazao yenyewe
hivyo kila mwananchi ametakiwa kukabiliana na hali ya bei ya bidhaa ambazo zimeonekana
zikipanda na nyingine kushuka.
Chanzo:
Dodoma FM.


Comments
Post a Comment