TWANGALA-KUPATA NAFASI BONGO MUVI NI KAZI
Msanii wa maigizo na bongo movie kutoka Dodoma Twangala amesema kupata fursa ya kuonyesha kipaji ulichonacho katika muvi ni kazi ngumu hivyo kupelekea watu kukata tama.
Amesema hayo wakati akizungumza na Beat Drive Show ya Dodoma fm ambapo amebainisha kuwa kuna watu wengi wanavipaji lakini kupata nafasi ni vigumu.
Akizungumzia kuhusu kupata fursa kwa upande wake amesema alianza katika matamasha mbalimbali ikiwepo katika tamasha la mtoto wa afrika ndipo baadae wakaunda kikundi cha maigizo.
Ameongeza kuwa jamii imekuwa ikiwachukulia waigizaji kama watu ambao hawataki kufanya kazi kitu ambacho sio kweli huku akisema kuna wasanii wengi ni maarufu na wana kipato cha juu.
Amemaliza kwa kuwataka wasanii kuwa na upendo na kuacha chuki binafsi hali inayoweza kupelekea kurudisha nyuma sanaa.
Miongoni mwa muvi alizofanya ni pamoja na Vanessa na mkono wa mungu
Na Beny Bert
GIFTED SON-MAMBO YALIKUWA MENGI,NDO MAANA NIMECHELEWA KUACHIA SHIDA
Msanii wa mziki wa Bongo fleva miondoko ya rap Gifted Son kutoka Dodoma ameeleza sababu zilizopelekea kuchelewa kwa video yake ya Shida kutoka kwenye albam yake ndogo ya shida.
Mwaka jana msanii huyo kutoka Biorn entertainment aliachia albam yake yenye nyimbo 5 ambayo inaenda kwa jina la shida.
Akizungumza na Beat Drive Show ya 98.4 Dodoma FM amesema video ya wimbo huoo imeandaliwa toka mwaka 2017 lakini walisimamisha zoezi la kuachia kazi hiyo kutokana na kazi mpya ambayo walipanga kuachia lakini mambo yaliingiliana.
Akizungumzia kuhusu nyimbo zingine ambazo hajatolewa video katika album hiyo amesema muda wowote anaweza akatoa kwa sababu anaamini bado ana muda wa kutosha.
Mwaka 2017 msanii huyo aliaachia album yake ndogo ambayo ilitajwa kuwa ni kazi iliyompa mpa sifa nzuri nje ya mipaka ya Tanzania ikiwepo Kenya Uganda mpaka nchi ya Zambia.
Na Beny Bert
ZIPORAH-JAMII YA KIAFRIKA HAIMPI NAFASI MWANAMKE
Msanii
wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma Zipora ameilaumu jamii kutokana
na kutoa nafasi kubwa kumsapoti mwanaume huku mwanamke akiachwa nyuma.
Ziporah
ni ni miongoni mwa wasanii wa kike ambao wanatajwa mara nyingi kwa kuwa
na kipaji cha mziki pamoja na sauti nzuri ya uimbaji.
Akizungumza
na Beat Drive Show amesema jamii kubwa ya kiafrika inatoa nafasi kubwa
kwa mwanaume bila kujua kuwa mwanamke ananafasi kubwa na anaweza kufanya
zaidi ya kile ambacho mwanaume anaweza kufanya.
Akizungumzia
kuhusu kuwepo kwa wasanii wachache wakike mkoani Dodoma amesema baadhi
yao ni waoga na baada ya kufanya kazi chache hawaoni umuhimu wakuendelea
kufanya kazi hiyo ili waendelee kuongeza ukubwa wa majina yao.
Hata
hivyo ametoa ushauri kwa watayarishaji wa mziki mkoani Dodoma
kutokuridhika hivyo kuongeza juhudi na jitihada ili waongeze ukubwa wa
kazi zao.
Ameongeza kuwa kwa mwaka 2018 ana mikakti ya
kuongeza ukubwa wa kazi zake ikiwa ni pamoja na kufanya kazi na
watayarishaji wa mziki kutoka nje ya mkoa wa Dodoma.
Na Beny Bert
MIRACLE NOUMA-KAZI YANGU IMEFANYA VIZURI
Msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma Miracle noma ameonesha kufurahishwa baada ya mapokezi mazuri ya kazi yake ambayo amemshirikisha Godzilla inayoenda kwa jina la ups and Down
Akizungumza na Dodoma fm amesema kazi yake imepokelewa vizuri kitu ambacho hakutegemea kama itakuwa hivyo
Akizungumzia kuhusu utofauti aliouona baada ya kumshirikisha Godzilla kwenye wimbo huo amesema ameongeza mashabiki wengi kutokana na msanii huyo kuwa na idadi kubwa ya watu wanaofatilia mziki wake
Hivi karibuni zilivuma tetesi huenda kundi ambalo yupo msanii huyo C.M.A limevunjika kutokana na muanzilishi wa kundi hilo Bin Laden kuwa bize na mambo yake kitu ambacho miracle amekataa sio kweli
Amemaliza kwa kusema kuwa wanasubiri kila mmoja atoe kazi yake kama solo artist ndipo kazi za kundi zitoke
Na Beny Bert
FIDELIS-WAONGOZAJI WA VIDEO SIO WABUNIFU
Waongozaji
wa video mkoani Dodoma wametakiwa kuwa wabunifu na kuongeza conection
ili kuleta ushindani wa video bora nchini na nje ya Tanzania.
Fidelis
ni miongoni mwa wasanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma amesema
waongozaji wengi wa video hawathamini kazi za wasanii kitu ambacho
hakitakiwi katika sanaa ya bongo fleva.
Amesema muongozaji anatakiwa amsaidie msanii kuweza kuongeza watu muhimu kitu ambacho kinahitaji nguvu kubwa.
Hivi
karibuni niliongea na moja kati ya waongozaji wa video Erick Backamaza
ambaye amefanya kazi mbalimbali zikiwemo baadhi ya video za jacobeat
alisema kwa waongozaji wapya wanaochipukia lazima wawe wabunifu ili
kuvutia soko la mziki wa bongo fleva.
Miongoni mwa waongozaji
wapya wanaofanya vizuri kutoka Dodoma ni pamoja na Nicklas ambaye
ameshoot wimbo wa roma zimbabwe pamoja na mikono juu wimbo wa nay wa
mitego.
Na Beny Bert Chanzo Dodoma Fm
YULE MKAKA-MSANII LAZIMA UJUE KUISOMA GAME INAHITAJI NINI
Kutokana na kubadilika kwa sanaa ya mziki wa bongo fleva nchini wasanii wametakiwa kubadilika ikiwa ni pamoja na kuto kutoa wimbo mara moja moja kwa kufanya hivyo itasaidia kukuza brand ya msanii.
Zamani ilikuwa ni vigumu kwa msanii kutoa wimbo kila baada ya mwezi mmoja lakini kwa kipindi hiki imekuwa ni jambo la kawaida katika tasnia ya mziki wa bongop fleva nchini.
Moja kati ya wasanii wanaofanya vizuri mkoani hapa Albert lakini jina lake la usanii ni YULE MKAKA amesema yeye ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitoa kazi moja na kusubiri kwa muda flani lakini sasa hivi ameamua kubadilika hiyo ni baada ya kusoma game ya bongofleva inataka kitu gani.
Amesema mara nyingi amekuwa akitumia hashtagi ibebe dodoma hii ni baada ya kuamini kuwa Dodoma kuna vipaji vingi ila tatizo ni kuwa seriazi na kujiamini ambapo amemtaja moni centrozone kama icon ya mkoa na kila kitu inawezekana endapo wasanii hao watakuwa na juhudi binafsi.
Amemaliza kwa kuwataka mashabiki wote kukaa mkao wa kula ambapo mda sio mrefu anakuja na kazi nyingine
Hivi karibuni Yule makaka ameachia kazi yake ambayo inaitwa kitochi.
SAL-MO BIORN NI MIONGONI MWA LEBO ZINAZOFANYA VIZURI
Msanii na mtayarishaji wa mziki wakizazi kipya Salmoo kutoka more feelings
production amesema baadhi ya lebo zilizopo mkoani hapa zina msaada mkubwa kwa
wasanii kwani kuna utofauti mkubwa kwa sasa ukitofautisha na zamani.
Salmoo amesema hayo wakti akizungumza na Dodoama Fm Radio ambapo ameitaja
lebo ya biorn kuwa ni miongoni mwa lebo inayowasimamia wasanii vizuri.
Akizungumzia kuhusu ukuaji wake katika kutayarisha mziki amesema
kumechangiwa na producer mwenzake melodies ambaye amehusika kwa kiasi kikubwa.
Hata hivyo amesema msanii hutakiwi kutegemea kufanya staili moja ya mziki
ila unatakiwa kuwa kila upande.
Hivi karibuni msanii huyo ameachia kazi yake mpya inayoitwa my wife
aliyomshirikisha jacobeat ambapo amesema anafanya utaratibu wa kushoot video
hadi kufika mwezi wa tatu itakuwa tayari.
Na Beny Bert
TWANGALA-KUPATA NAFASI BONGO MUVI NI KAZI
Msanii wa maigizo na bongo movie kutoka Dodoma Twangala amesema kupata fursa ya kuonyesha kipaji ulichonacho katika muvi ni kazi ngumu hivyo kupelekea watu kukata tama.
Amesema hayo wakati akizungumza na Beat Drive Show ya Dodoma fm ambapo amebainisha kuwa kuna watu wengi wanavipaji lakini kupata nafasi ni vigumu.
Akizungumzia kuhusu kupata fursa kwa upande wake amesema alianza katika matamasha mbalimbali ikiwepo katika tamasha la mtoto wa afrika ndipo baadae wakaunda kikundi cha maigizo.
Ameongeza kuwa jamii imekuwa ikiwachukulia waigizaji kama watu ambao hawataki kufanya kazi kitu ambacho sio kweli huku akisema kuna wasanii wengi ni maarufu na wana kipato cha juu.
Amemaliza kwa kuwataka wasanii kuwa na upendo na kuacha chuki binafsi hali inayoweza kupelekea kurudisha nyuma sanaa.
Miongoni mwa muvi alizofanya ni pamoja na Vanessa na mkono wa mungu
Na Beny Bert
GIFTED SON-MAMBO YALIKUWA MENGI,NDO MAANA NIMECHELEWA KUACHIA SHIDA
Msanii wa mziki wa Bongo fleva miondoko ya rap Gifted Son kutoka Dodoma ameeleza sababu zilizopelekea kuchelewa kwa video yake ya Shida kutoka kwenye albam yake ndogo ya shida.
Mwaka jana msanii huyo kutoka Biorn entertainment aliachia albam yake yenye nyimbo 5 ambayo inaenda kwa jina la shida.
Akizungumza na Beat Drive Show ya 98.4 Dodoma FM amesema video ya wimbo huoo imeandaliwa toka mwaka 2017 lakini walisimamisha zoezi la kuachia kazi hiyo kutokana na kazi mpya ambayo walipanga kuachia lakini mambo yaliingiliana.
Akizungumzia kuhusu nyimbo zingine ambazo hajatolewa video katika album hiyo amesema muda wowote anaweza akatoa kwa sababu anaamini bado ana muda wa kutosha.
Mwaka 2017 msanii huyo aliaachia album yake ndogo ambayo ilitajwa kuwa ni kazi iliyompa mpa sifa nzuri nje ya mipaka ya Tanzania ikiwepo Kenya Uganda mpaka nchi ya Zambia.
Na Beny Bert
ZIPORAH-JAMII YA KIAFRIKA HAIMPI NAFASI MWANAMKE
Msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma Zipora ameilaumu jamii kutokana na kutoa nafasi kubwa kumsapoti mwanaume huku mwanamke akiachwa nyuma.
Ziporah ni ni miongoni mwa wasanii wa kike ambao wanatajwa mara nyingi kwa kuwa na kipaji cha mziki pamoja na sauti nzuri ya uimbaji.
Akizungumza na Beat Drive Show amesema jamii kubwa ya kiafrika inatoa nafasi kubwa kwa mwanaume bila kujua kuwa mwanamke ananafasi kubwa na anaweza kufanya zaidi ya kile ambacho mwanaume anaweza kufanya.
Akizungumzia kuhusu kuwepo kwa wasanii wachache wakike mkoani Dodoma amesema baadhi yao ni waoga na baada ya kufanya kazi chache hawaoni umuhimu wakuendelea kufanya kazi hiyo ili waendelee kuongeza ukubwa wa majina yao.
Hata hivyo ametoa ushauri kwa watayarishaji wa mziki mkoani Dodoma kutokuridhika hivyo kuongeza juhudi na jitihada ili waongeze ukubwa wa kazi zao.
Ameongeza kuwa kwa mwaka 2018 ana mikakti ya kuongeza ukubwa wa kazi zake ikiwa ni pamoja na kufanya kazi na watayarishaji wa mziki kutoka nje ya mkoa wa Dodoma.
Na Beny Bert
MIRACLE NOUMA-KAZI YANGU IMEFANYA VIZURI
Msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma Miracle noma ameonesha kufurahishwa baada ya mapokezi mazuri ya kazi yake ambayo amemshirikisha Godzilla inayoenda kwa jina la ups and Down
Akizungumza na Dodoma fm amesema kazi yake imepokelewa vizuri kitu ambacho hakutegemea kama itakuwa hivyo
Akizungumzia kuhusu utofauti aliouona baada ya kumshirikisha Godzilla kwenye wimbo huo amesema ameongeza mashabiki wengi kutokana na msanii huyo kuwa na idadi kubwa ya watu wanaofatilia mziki wake
Hivi karibuni zilivuma tetesi huenda kundi ambalo yupo msanii huyo C.M.A limevunjika kutokana na muanzilishi wa kundi hilo Bin Laden kuwa bize na mambo yake kitu ambacho miracle amekataa sio kweli
Amemaliza kwa kusema kuwa wanasubiri kila mmoja atoe kazi yake kama solo artist ndipo kazi za kundi zitoke
Na Beny Bert
FIDELIS-WAONGOZAJI WA VIDEO SIO WABUNIFU
Waongozaji wa video mkoani Dodoma wametakiwa kuwa wabunifu na kuongeza conection ili kuleta ushindani wa video bora nchini na nje ya Tanzania.
Fidelis ni miongoni mwa wasanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma amesema waongozaji wengi wa video hawathamini kazi za wasanii kitu ambacho hakitakiwi katika sanaa ya bongo fleva.
Amesema muongozaji anatakiwa amsaidie msanii kuweza kuongeza watu muhimu kitu ambacho kinahitaji nguvu kubwa.
Hivi
karibuni niliongea na moja kati ya waongozaji wa video Erick Backamaza
ambaye amefanya kazi mbalimbali zikiwemo baadhi ya video za jacobeat
alisema kwa waongozaji wapya wanaochipukia lazima wawe wabunifu ili
kuvutia soko la mziki wa bongo fleva.
Miongoni mwa waongozaji wapya wanaofanya vizuri kutoka Dodoma ni pamoja na Nicklas ambaye ameshoot wimbo wa roma zimbabwe pamoja na mikono juu wimbo wa nay wa mitego.
Na Beny Bert Chanzo Dodoma Fm
YULE MKAKA-MSANII LAZIMA UJUE KUISOMA GAME INAHITAJI NINI
Kutokana na kubadilika kwa sanaa ya mziki wa bongo fleva nchini wasanii wametakiwa kubadilika ikiwa ni pamoja na kuto kutoa wimbo mara moja moja kwa kufanya hivyo itasaidia kukuza brand ya msanii.
Zamani ilikuwa ni vigumu kwa msanii kutoa wimbo kila baada ya mwezi mmoja lakini kwa kipindi hiki imekuwa ni jambo la kawaida katika tasnia ya mziki wa bongop fleva nchini.
Moja kati ya wasanii wanaofanya vizuri mkoani hapa Albert lakini jina lake la usanii ni YULE MKAKA amesema yeye ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitoa kazi moja na kusubiri kwa muda flani lakini sasa hivi ameamua kubadilika hiyo ni baada ya kusoma game ya bongofleva inataka kitu gani.
Amesema mara nyingi amekuwa akitumia hashtagi ibebe dodoma hii ni baada ya kuamini kuwa Dodoma kuna vipaji vingi ila tatizo ni kuwa seriazi na kujiamini ambapo amemtaja moni centrozone kama icon ya mkoa na kila kitu inawezekana endapo wasanii hao watakuwa na juhudi binafsi.
Amemaliza kwa kuwataka mashabiki wote kukaa mkao wa kula ambapo mda sio mrefu anakuja na kazi nyingine
Hivi karibuni Yule makaka ameachia kazi yake ambayo inaitwa kitochi.
SAL-MO BIORN NI MIONGONI MWA LEBO ZINAZOFANYA VIZURI
Comments
Post a Comment